Surah Al-Muddaththir (undefined) is the 74th chapter of the Holy Quran. It was revealed in Mecca and contains 56 verses (ayahs). Read it below with the Arabic text, transliteration, and Swahili translation, or open it as interactive flashcards to memorize it verse by verse.
- 74:1
يَٰٓأَيُّهَا ٱلْمُدَّثِّرُ
Yaaa ayyuhal muddassir
Ewe uliye jigubika!
- 74:2
قُمْ فَأَنذِرْ
Qum fa anzir
Simama uonye!
- 74:3
وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ
Wa rabbaka fakabbir
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
- 74:4
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ
Wa siyaabaka fatahhir
Na nguo zako, zisafishe.
- 74:5
وَٱلرُّجْزَ فَٱهْجُرْ
Warrujza fahjur
Na yaliyo machafu yahame!
- 74:6
وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ
Wa laa tamnun tastaksir
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
- 74:7
وَلِرَبِّكَ فَٱصْبِرْ
Wa li Rabbika fasbir
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
- 74:8
فَإِذَا نُقِرَ فِى ٱلنَّاقُورِ
Fa izaa nuqira fin naaqoor
Basi litapo pulizwa barugumu,
- 74:9
فَذَٰلِكَ يَوْمَئِذٍۢ يَوْمٌ عَسِيرٌ
Fazaalika yawma 'iziny yawmun 'aseer
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
- 74:10
عَلَى ٱلْكَٰفِرِينَ غَيْرُ يَسِيرٍۢ
'Alal kaafireena ghayru yaseer
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
- 74:11
ذَرْنِى وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًۭا
Zamee wa man khalaqtu waheedaa
Niache peke yangu na niliye muumba;
- 74:12
وَجَعَلْتُ لَهُۥ مَالًۭا مَّمْدُودًۭا
Wa ja'altu lahoo maalam mamdoodaa
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
- 74:13
وَبَنِينَ شُهُودًۭا
Wa baneena shuhoodaa
Na wana wanao onekana,
- 74:14
وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمْهِيدًۭا
Wa mahhattu lahoo tamheeda
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
- 74:15
ثُمَّ يَطْمَعُ أَنْ أَزِيدَ
Summa yat ma'u an azeed
Kisha anatumai nimzidishie!
- 74:16
كَلَّآ ۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِءَايَٰتِنَا عَنِيدًۭا
Kallaaa innahoo kaana li Aayaatinaa 'aneedaa
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
- 74:17
سَأُرْهِقُهُۥ صَعُودًا
Sa urhiquhoo sa'oodaa
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
- 74:18
إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ
Innahoo fakkara wa qaddar
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
- 74:19
فَقُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ
Faqutila kayfa qaddar
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
- 74:20
ثُمَّ قُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ
Summa qutila kaifa qaddar
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
- 74:21
ثُمَّ نَظَرَ
Summa nazar
Kisha akatazama,
- 74:22
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Summa 'abasa wa basar
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
- 74:23
ثُمَّ أَدْبَرَ وَٱسْتَكْبَرَ
Summaa adbara wastakbar
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
- 74:24
فَقَالَ إِنْ هَٰذَآ إِلَّا سِحْرٌۭ يُؤْثَرُ
Faqaala in haazaaa illaa sihruny yu'sar
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
- 74:25
إِنْ هَٰذَآ إِلَّا قَوْلُ ٱلْبَشَرِ
In haazaaa illaa qawlul bashar
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
- 74:26
سَأُصْلِيهِ سَقَرَ
Sa usleehi saqar
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
- 74:27
وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سَقَرُ
Wa maaa adraaka maa saqar
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
- 74:28
لَا تُبْقِى وَلَا تَذَرُ
Laa tubqee wa laa tazar
Haubakishi wala hausazi.
- 74:29
لَوَّاحَةٌۭ لِّلْبَشَرِ
Lawwaahatul lilbashar
Unababua ngozi iwe nyeusi.
- 74:30
عَلَيْهَا تِسْعَةَ عَشَرَ
'Alaihaa tis'ata 'ashar
Juu yake wapo kumi na tisa.
- 74:31
وَمَا جَعَلْنَآ أَصْحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةًۭ ۙ وَمَا جَعَلْنَا عِدَّتَهُمْ إِلَّا فِتْنَةًۭ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لِيَسْتَيْقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُوا۟ ٱلْكِتَٰبَ وَيَزْدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓا۟ إِيمَٰنًۭا ۙ وَلَا يَرْتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُوا۟ ٱلْكِتَٰبَ وَٱلْمُؤْمِنُونَ ۙ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِى قُلُوبِهِم مَّرَضٌۭ وَٱلْكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلًۭا ۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهْدِى مَن يَشَآءُ ۚ وَمَا يَعْلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَ ۚ وَمَا هِىَ إِلَّا ذِكْرَىٰ لِلْبَشَرِ
Wa maaja''alnaaa As haaban naari illaa malaaa 'ikatanw wa maa ja'alnaa 'iddatahum illaa fitnatal lillazeena kafaroo liyastayqinal lazeena ootul kitaaba wa yazdaadal lazeena aamanooo eemaananw wa laa yartaabal lazeena ootul kitaaba walmu'minoona wa liyaqoolal lazeena fee quloo bihim maradunw walkaafiroona maazaaa araadal laahu bihaazaa masalaa; kazaalika yudillul laahu many yashaaa'u wa yahdee many yashaaa'; wa maa ya'lamu junooda rabbika illaa hoo; wa maa hiya illaa zikraa lil bashar
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
- 74:32
كَلَّا وَٱلْقَمَرِ
Kallaa walqamar
Hasha! Naapa kwa mwezi!
- 74:33
وَٱلَّيْلِ إِذْ أَدْبَرَ
Wallaili adbar
Na kwa usiku unapo kucha!
- 74:34
وَٱلصُّبْحِ إِذَآ أَسْفَرَ
Wassub hi izaaa asfar
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
- 74:35
إِنَّهَا لَإِحْدَى ٱلْكُبَرِ
Innahaa la ihdal kubar
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
- 74:36
نَذِيرًۭا لِّلْبَشَرِ
Nazeeral lilbashar
Ni onyo kwa binaadamu,
- 74:37
لِمَن شَآءَ مِنكُمْ أَن يَتَقَدَّمَ أَوْ يَتَأَخَّرَ
Liman shaaa'a minkum any yataqaddama aw yata akhkhar
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
- 74:38
كُلُّ نَفْسٍۭ بِمَا كَسَبَتْ رَهِينَةٌ
Kullu nafsim bim kasabat raheenah
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
- 74:39
إِلَّآ أَصْحَٰبَ ٱلْيَمِينِ
Illaaa as haabal yameen
Isipo kuwa watu wa kuliani.
- 74:40
فِى جَنَّٰتٍۢ يَتَسَآءَلُونَ
Fee jannaatiny yata saaa'aloon
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
- 74:41
عَنِ ٱلْمُجْرِمِينَ
'Anil mujrimeen
Khabari za wakosefu:
- 74:42
مَا سَلَكَكُمْ فِى سَقَرَ
Maa salakakum fee saqar
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
- 74:43
قَالُوا۟ لَمْ نَكُ مِنَ ٱلْمُصَلِّينَ
Qaaloo lam naku minal musalleen
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.
- 74:44
وَلَمْ نَكُ نُطْعِمُ ٱلْمِسْكِينَ
Wa lam naku nut'imul miskeen
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
- 74:45
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلْخَآئِضِينَ
Wa kunnaa nakhoodu ma'al khaaa'ideen
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
- 74:46
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ
Wa kunnaa nukazzibu bi yawmid Deen
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
- 74:47
حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلْيَقِينُ
Hattaaa ataanal yaqeen
Mpaka yakini ilipo tufikia.
- 74:48
فَمَا تَنفَعُهُمْ شَفَٰعَةُ ٱلشَّٰفِعِينَ
Famaa tanfa'uhum shafaa'atush shaafi'een
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
- 74:49
فَمَا لَهُمْ عَنِ ٱلتَّذْكِرَةِ مُعْرِضِينَ
Famaa lahum 'anittazkirati mu'rideen
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
- 74:50
كَأَنَّهُمْ حُمُرٌۭ مُّسْتَنفِرَةٌۭ
Ka annahum humurum mustanfirah
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
- 74:51
فَرَّتْ مِن قَسْوَرَةٍۭ
Farrat min qaswarah
Wanao mkimbia simba!
- 74:52
بَلْ يُرِيدُ كُلُّ ٱمْرِئٍۢ مِّنْهُمْ أَن يُؤْتَىٰ صُحُفًۭا مُّنَشَّرَةًۭ
Bal yureedu kullum ri'im minhum any yu'taa suhufam munashsharah
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
- 74:53
كَلَّا ۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلْءَاخِرَةَ
Kallaa bal laa yakhaafoonal aakhirah
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
- 74:54
كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذْكِرَةٌۭ
Kallaaa innahoo tazkirah
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
- 74:55
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Fa man shaaa'a zakarah
Basi anaye taka atakumbuka.
- 74:56
وَمَا يَذْكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ ۚ هُوَ أَهْلُ ٱلتَّقْوَىٰ وَأَهْلُ ٱلْمَغْفِرَةِ
Wa maa yazkuroona illaaa any yashaaa'al laah; Huwa ahlut taqwaa wa ahlul maghfirah
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
About Surah Al-Muddaththir
Al-Muddaththir, the Cloaked One, contains some of the earliest revelation, calling the Prophet (peace be upon him) to rise and warn, to magnify his Lord, and to keep himself pure. It warns the arrogant who plotted against the message and describes the regret of those who neglected prayer and feeding the poor.
Themes: The call to warn, Purity, Arrogance and its end, Prayer and charity
Arabic: Uthmani script (Hafs). Translation: Swahili. Recitation: Mishary Rashid Alafasy. See Sources for full attribution.