All Surahs

Surah Ash-Shu'ara (undefined)

سُورَةُ الشُّعَرَاءِ

Surah 26 of the Holy Quran · Meccan · 227 verses

Also spelled: Shu'ara, Ash Shu'ara, AshShu'ara, The Poets

Surah Ash-Shu'ara (undefined) is the 26th chapter of the Holy Quran. It was revealed in Mecca and contains 227 verses (ayahs). Read it below with the Arabic text, transliteration, and Swahili translation, or open it as interactive flashcards to memorize it verse by verse.

  1. 26:1

    طسٓمٓ

    Taa-Seeen-Meeem

    T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)

  2. 26:2

    تِلْكَ ءَايَٰتُ ٱلْكِتَٰبِ ٱلْمُبِينِ

    Tilka Aayaatul Kitaabil Mubeen

    Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.

  3. 26:3

    لَعَلَّكَ بَٰخِعٌۭ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ

    La'allaka baakhi'un nafsaka allaa yakoonoo mu'mineen

    Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.

  4. 26:4

    إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةًۭ فَظَلَّتْ أَعْنَٰقُهُمْ لَهَا خَٰضِعِينَ

    In nashaa nunazzil 'alaihim minas samaaa'i Aayatan fazallat a'naaquhum lahaa khaadi'een

    Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.

  5. 26:5

    وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍۢ مِّنَ ٱلرَّحْمَٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا۟ عَنْهُ مُعْرِضِينَ

    Wa maa yaateehim min zikrim minar Rahmaani muhdasin illaa kaanoo 'anhu mu'rideen

    Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.

  6. 26:6

    فَقَدْ كَذَّبُوا۟ فَسَيَأْتِيهِمْ أَنۢبَٰٓؤُا۟ مَا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ

    Faqad kazzaboo fasa yaateehim ambaaa'u maa kaanoo bihee yastahzi'oon

    Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.

  7. 26:7

    أَوَلَمْ يَرَوْا۟ إِلَى ٱلْأَرْضِ كَمْ أَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍۢ كَرِيمٍ

    Awa lam yaraw ilal ardi kam ambatnaa feehaa min kulli zawjin kareem

    Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?

  8. 26:8

    إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

    Inn fee zaalika la Aayah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

    Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

  9. 26:9

    وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

    Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

    Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

  10. 26:10

    وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئْتِ ٱلْقَوْمَ ٱلظَّٰلِمِينَ

    Wa iz naadaa Rabbuka Moosaaa ani'-til qawmaz zaalimeen

    Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,

  11. 26:11

    قَوْمَ فِرْعَوْنَ ۚ أَلَا يَتَّقُونَ

    Qawma Fir'awn; alaa yattaqoon

    Watu wa Firauni. Hawaogopi?

  12. 26:12

    قَالَ رَبِّ إِنِّىٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ

    Qaala Rabbi inneee akhaafu ai yukazziboon

    Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.

  13. 26:13

    وَيَضِيقُ صَدْرِى وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِى فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَٰرُونَ

    Wa yadeequ sadree wa laa yantaliqu lisaanee fa arsil ilaa Haaroon

    Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.

  14. 26:14

    وَلَهُمْ عَلَىَّ ذَنۢبٌۭ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ

    Wa lahum 'alaiya zambun fa akhaafu ai yaqtuloon

    Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.

  15. 26:15

    قَالَ كَلَّا ۖ فَٱذْهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآ ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ

    Qaala kallaa fazhabaa bi Aayaatinaaa innaa ma'akum mustami'oon

    Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.

  16. 26:16

    فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Faatiyaa Fir'awna faqoolaaa innaa Rasoolu Rabbil 'aalameen

    Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  17. 26:17

    أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ

    An arsil ma'anaa Baneee Israaa'eel

    Waachilie Wana wa Israili wende nasi.

  18. 26:18

    قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًۭا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ

    Qaala alam nurabbika feenaa waleedanw wa labista feenaa min 'umurika sineen

    (Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?

  19. 26:19

    وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ ٱلَّتِى فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلْكَٰفِرِينَ

    Wa fa'alta fa'latakal latee fa'alta wa anta minal kaafireen

    Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?

  20. 26:20

    قَالَ فَعَلْتُهَآ إِذًۭا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

    Qaala fa'altuhaaa izanw wa ana minad daaaleen

    (Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.

  21. 26:21

    فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِى رَبِّى حُكْمًۭا وَجَعَلَنِى مِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ

    Fafarartu minkum lam maa khiftukum fawahaba lee Rabbee hukmanw wa ja'alanee minal mursaleen

    Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.

  22. 26:22

    وَتِلْكَ نِعْمَةٌۭ تَمُنُّهَا عَلَىَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ

    Wa tilka ni'matun tamun nuhaa 'alaiya an 'abbatta Baneee Israaa'eel

    Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?

  23. 26:23

    قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Qaala Fir'awnu wa maa Rabbul 'aalameen

    Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?

  24. 26:24

    قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ

    Qaala Rabbus samaawaati wal ardi wa maa bainahumaa in kuntum mooqineen

    Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.

  25. 26:25

    قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُۥٓ أَلَا تَسْتَمِعُونَ

    Qaala liman hawlahooo alaa tastami'oon

    (Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?

  26. 26:26

    قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ

    Qaala Rabbukum wa Rabbu aabaaa'ikumul awwaleen

    (Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.

  27. 26:27

    قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِىٓ أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌۭ

    Qaala inna Rasoolakumul lazee ursila ilaikum lamajnoon

    (Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.

  28. 26:28

    قَالَ رَبُّ ٱلْمَشْرِقِ وَٱلْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَآ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ

    Qaala Rabbul mashriqi wal maghribi wa maa baina humaa in kuntum ta'qiloon

    (Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.

  29. 26:29

    قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذْتَ إِلَٰهًا غَيْرِى لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ ٱلْمَسْجُونِينَ

    Qaala la'init takhazta ilaahan ghairee la aj'alannaka minal masjooneen

    (Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.

  30. 26:30

    قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَىْءٍۢ مُّبِينٍۢ

    Qaala awalw ji'tuka bishai'im mubeen

    Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?

  31. 26:31

    قَالَ فَأْتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

    Qaala faati biheee in kunta minas saadiqeen

    Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.

  32. 26:32

    فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ ثُعْبَانٌۭ مُّبِينٌۭ

    Fa alqaa 'asaahu fa izaaa hiya su'baanum mubeen

    Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.

  33. 26:33

    وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِىَ بَيْضَآءُ لِلنَّٰظِرِينَ

    Wa naza'a yadahoo faizaa hiya baidaaa'u linnaa zireen

    Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.

  34. 26:34

    قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٌۭ

    Qaala lilmala-i hawlahooo inna haazaa lasaahirun 'aleem

    (Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.

  35. 26:35

    يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِۦ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ

    Yureedu ai yukhrijakum min ardikum bisihrihee famaazaa taamuroon

    Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?

  36. 26:36

    قَالُوٓا۟ أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَٱبْعَثْ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

    Qaalooo arjih wa akhaahu wab'as filmadaaa'ini haashireen

    Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.

  37. 26:37

    يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍۢ

    Yaatooka bikulli sah haarin 'aleem

    Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.

  38. 26:38

    فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوْمٍۢ مَّعْلُومٍۢ

    Fa jumi'as saharatu limeeqaati Yawmim ma'loom

    Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.

  39. 26:39

    وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ

    Wa qeela linnaasi hal antum mujtami'oon

    Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?

  40. 26:40

    لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَٰلِبِينَ

    La'allanaa nattabi'us saharata in kaanoo humul ghaalibeen

    Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.

  41. 26:41

    فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُوا۟ لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ ٱلْغَٰلِبِينَ

    Falammaa jaaa'as saharatu qaaloo li Fir'awna a'inna lanaa la ajjran in kunnaa nahnul ghaalibeen

    Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?

  42. 26:42

    قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًۭا لَّمِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ

    Qaala na'am wa innakum izal laminal muqarrabeen

    Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.

  43. 26:43

    قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلْقُوا۟ مَآ أَنتُم مُّلْقُونَ

    Qaala lahum Moosaaa alqoo maaa antum mulqoon

    Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.

  44. 26:44

    فَأَلْقَوْا۟ حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا۟ بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ ٱلْغَٰلِبُونَ

    Fa alqaw hibaalahum wa 'isiyyahum wa qaaloo bi'izzati Fir'awna innaa lanahnul ghaaliboon

    Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.

  45. 26:45

    فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ

    Fa alqaa Moosaa 'asaahu fa izaa hiya talqafu maa yaafikoon

    Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.

  46. 26:46

    فَأُلْقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ

    Fa ulqiyas saharatu saajideen

    Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.

  47. 26:47

    قَالُوٓا۟ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Qaalooo aamannaa bi Rabbil 'aalameen

    Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  48. 26:48

    رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

    Rabbi Moosaa wa Haaroon

    Mola Mlezi wa Musa na Harun.

  49. 26:49

    قَالَ ءَامَنتُمْ لَهُۥ قَبْلَ أَنْ ءَاذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِى عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَٰفٍۢ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ

    Qaala aamantum lahoo qabla an aazana lakum innahoo lakabeerukumul lazee 'alla makumus sihra falasawfa ta'lamoon; la uqatti'anna aidiyakum wa arjulakum min khilaafinw wa la usallibanna kum ajma'een

    (Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.

  50. 26:50

    قَالُوا۟ لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ

    Qaaloo la daira innaaa ilaa Rabbinaa munqalliboon

    Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

  51. 26:51

    إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

    Innaa natma'u ai yaghfira lanaa Rabbunna khataa yaanaaa an kunnaaa awwalal mu'mineen

    Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.

  52. 26:52

    ۞ وَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِىٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

    Wa awhainaaa ilaa Moosaaa an asri bi'ibaadeee innakum muttaba'oon

    Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.

  53. 26:53

    فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

    Fa arsala Fir'awnu filmadaaa'ini haashireen

    Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.

  54. 26:54

    إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَشِرْذِمَةٌۭ قَلِيلُونَ

    Inna haaa'ulaaa'i lashir zimatun qaleeloon

    (Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.

  55. 26:55

    وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَآئِظُونَ

    Wa innahum lanaa laghaaa'izoon

    Nao wanatuudhi.

  56. 26:56

    وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ

    Wa innaa lajamee'un haaziroon

    Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.

  57. 26:57

    فَأَخْرَجْنَٰهُم مِّن جَنَّٰتٍۢ وَعُيُونٍۢ

    Fa akhrajnaahum min Jannaatinw wa 'uyoon

    Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,

  58. 26:58

    وَكُنُوزٍۢ وَمَقَامٍۢ كَرِيمٍۢ

    Wa kunoozinw wa ma qaamin kareem

    Na makhazina, na vyeo vya hishima,

  59. 26:59

    كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَٰهَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ

    Kazaalika wa awrasnaahaa Baneee Israaa'eel

    Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.

  60. 26:60

    فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ

    Fa atba'oohum mushriqeen

    Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.

  61. 26:61

    فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ

    Falammaa taraaa'al jam'aani qaala as haabu Moosaaa innaa lamudrakoon

    Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!

  62. 26:62

    قَالَ كَلَّآ ۖ إِنَّ مَعِىَ رَبِّى سَيَهْدِينِ

    Qaala kallaaa inna ma'iya Rabbee sa yahdeen

    (Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!

  63. 26:63

    فَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضْرِب بِّعَصَاكَ ٱلْبَحْرَ ۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍۢ كَٱلطَّوْدِ ٱلْعَظِيمِ

    Fa awhainaaa ilaa Moosaaa anidrib bi'asaakal bahra fanfalaqa fakaana kullu firqin kattawdil 'azeem

    Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.

  64. 26:64

    وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ ٱلْءَاخَرِينَ

    Wa azlafnaa sammal aakhareen

    Na tukawajongeza hapo wale wengine.

  65. 26:65

    وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجْمَعِينَ

    Wa anjainaa Moosaa wa mam ma'ahooo ajma'een

    Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.

  66. 26:66

    ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْءَاخَرِينَ

    Summa aghraqnal aakhareen

    Kisha tukawazamisha hao wengine.

  67. 26:67

    إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

    Inna fee zaalika la Aayaah; wa maa kaana aksaru hu mu'mineen

    Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.

  68. 26:68

    وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

    Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

    Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

  69. 26:69

    وَٱتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَٰهِيمَ

    Watlu 'alaihim naba-a Ibraaheem

    Na wasomee khabari za Ibrahim.

  70. 26:70

    إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَا تَعْبُدُونَ

    Iz qaala li abeehi wa qawmihee maa ta'budoon

    Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?

  71. 26:71

    قَالُوا۟ نَعْبُدُ أَصْنَامًۭا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ

    Qaaloo na'budu asnaaman fanazallu lahaa 'aakifeen

    Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.

  72. 26:72

    قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ

    Qaala hal yasma'oona kum iz tad'oon

    Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?

  73. 26:73

    أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ

    Aw yanfa'oonakum aw yadurroon

    Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?

  74. 26:74

    قَالُوا۟ بَلْ وَجَدْنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ

    Qaaloo bal wajadnaaa aabaaa 'anaa kazaalika yaf'aloon

    Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.

  75. 26:75

    قَالَ أَفَرَءَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ

    Qaala afara 'aitum maa kuntum ta'budoon

    Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-

  76. 26:76

    أَنتُمْ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلْأَقْدَمُونَ

    Antum wa aabaaa'ukumul aqdamoon

    Nyinyi na baba zenu wa zamani?

  77. 26:77

    فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّۭ لِّىٓ إِلَّا رَبَّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Fa innahum 'aduwwwul leee illaa Rabbal 'aalameen

    Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  78. 26:78

    ٱلَّذِى خَلَقَنِى فَهُوَ يَهْدِينِ

    Allazee khalaqanee fa Huwa yahdeen

    Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,

  79. 26:79

    وَٱلَّذِى هُوَ يُطْعِمُنِى وَيَسْقِينِ

    Wallazee Huwa yut'imunee wa yasqeen

    Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.

  80. 26:80

    وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ

    Wa izaa mardtu fahuwa yashfeen

    Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.

  81. 26:81

    وَٱلَّذِى يُمِيتُنِى ثُمَّ يُحْيِينِ

    Wallazee yumeetunee summa yuhyeen

    Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.

  82. 26:82

    وَٱلَّذِىٓ أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِى خَطِيٓـَٔتِى يَوْمَ ٱلدِّينِ

    Wallazeee atma'u ai yaghfira lee khateee' atee Yawmad Deen

    Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.

  83. 26:83

    رَبِّ هَبْ لِى حُكْمًۭا وَأَلْحِقْنِى بِٱلصَّٰلِحِينَ

    Rabbi hab lee hukmanw wa alhiqnee bis saaliheen

    Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.

  84. 26:84

    وَٱجْعَل لِّى لِسَانَ صِدْقٍۢ فِى ٱلْءَاخِرِينَ

    Waj'al lee lisaana sidqin fil aakhireen

    Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.

  85. 26:85

    وَٱجْعَلْنِى مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ

    Waj'alnee minw warasati Jannnatin Na'eem

    Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.

  86. 26:86

    وَٱغْفِرْ لِأَبِىٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

    Waghfir li abeee innahoo kaana mind daalleen

    Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.

  87. 26:87

    وَلَا تُخْزِنِى يَوْمَ يُبْعَثُونَ

    Wa laa tukhzinee Yawma yub'asoon

    Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.

  88. 26:88

    يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌۭ وَلَا بَنُونَ

    Yawma laa yanfa'u maalunw wa laa banoon

    Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.

  89. 26:89

    إِلَّا مَنْ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلْبٍۢ سَلِيمٍۢ

    Illaa man atal laaha biqalbin saleem

    Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.

  90. 26:90

    وَأُزْلِفَتِ ٱلْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ

    Wa uzlifatil Jannatu lilmuttaqeen

    Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.

  91. 26:91

    وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ

    Wa burrizatil Jaheemu lilghaaween

    Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.

  92. 26:92

    وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ

    Wa qeela lahum aina maa kuntum ta'budoon

    Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu

  93. 26:93

    مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ

    Min doonil laahi hal yansuroonakum aw yantasiroon

    Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?

  94. 26:94

    فَكُبْكِبُوا۟ فِيهَا هُمْ وَٱلْغَاوُۥنَ

    Fakubkiboo feehaa hum walghaawoon

    Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,

  95. 26:95

    وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ

    Wa junoodu Ibleesa ajma'oon

    Na majeshi ya Ibilisi yote.

  96. 26:96

    قَالُوا۟ وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ

    Qaaloo wa hum feehaa yakkhtasimoon

    Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:

  97. 26:97

    تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِى ضَلَٰلٍۢ مُّبِينٍ

    Tallaahi in kunnaa lafee dalaalim mubeen

    Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,

  98. 26:98

    إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Iz nusawweekum bi Rabbil 'aalameen

    Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  99. 26:99

    وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلْمُجْرِمُونَ

    Wa maaa adallanaaa illal mujrimoon

    Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.

  100. 26:100

    فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ

    Famaa lanaa min shaa fi'een

    Basi hatuna waombezi.

  101. 26:101

    وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍۢ

    Wa laa sadeeqin hameem

    Wala rafiki wa dhati.

  102. 26:102

    فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةًۭ فَنَكُونَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

    Falaw anna lanaa karratan fanakoona minal mu'mineen

    Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.

  103. 26:103

    إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

    Inna fee zaalika la Aayatanw wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

    Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

  104. 26:104

    وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

    Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

    Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

  105. 26:105

    كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ ٱلْمُرْسَلِينَ

    Kazzabat qawmu Noohinil Mursaleen

    Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.

  106. 26:106

    إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

    Iz qaala lahum akhoohum Noohun alaa tattaqoon

    Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?

  107. 26:107

    إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

    Innee lakum Rasoolun ameen

    Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

  108. 26:108

    فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

    Fattaqullaaha wa atee'oon

    Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

  109. 26:109

    وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Wa maaa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

    Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  110. 26:110

    فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

    Fattaqul laaha wa atee'oon

    Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

  111. 26:111

    ۞ قَالُوٓا۟ أَنُؤْمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلْأَرْذَلُونَ

    Qaalooo anu'minu laka wattaba 'akal arzaloon

    Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?

  112. 26:112

    قَالَ وَمَا عِلْمِى بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ

    Qaala wa maa 'ilmee bimaa kaanoo ya'maloon

    Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?

  113. 26:113

    إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّى ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ

    In hisaabuhum illaa 'alaa Rabbee law tash'uroon

    Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!

  114. 26:114

    وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلْمُؤْمِنِينَ

    Wa maaa ana bitaaridil mu'mineen

    Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.

  115. 26:115

    إِنْ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٌۭ مُّبِينٌۭ

    In ana illaa nazeerum mubeen

    Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.

  116. 26:116

    قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمَرْجُومِينَ

    Qaaloo la'il lam tantahi yaa Noohu latakoonanna minal marjoomeen

    Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.

  117. 26:117

    قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِى كَذَّبُونِ

    Qaala Rabbi inna qawmee kazzaboon

    Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.

  118. 26:118

    فَٱفْتَحْ بَيْنِى وَبَيْنَهُمْ فَتْحًۭا وَنَجِّنِى وَمَن مَّعِىَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

    Faftab bainee wa bai nahum fat hanw wa najjinee wa mam ma'iya minal mu'mineen

    Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.

  119. 26:119

    فَأَنجَيْنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ

    Fa anjainaahu wa mamma'ahoo fil fulkil mashhoon

    Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.

  120. 26:120

    ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ ٱلْبَاقِينَ

    Summa aghraqnaa ba'dul baaqeen

    Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.

  121. 26:121

    إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

    Inna fee zaalika la Aayaah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

    Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.

  122. 26:122

    وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

    Wa inna Rabbaka la huwal 'Azeezur Raheem

    Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

  123. 26:123

    كَذَّبَتْ عَادٌ ٱلْمُرْسَلِينَ

    Kazzabat 'Aadunil mursaleen

    Kina A'd waliwakanusha Mitume.

  124. 26:124

    إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ

    Iz qaala lahum akhoohum Hoodun alaa tattaqoon

    Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?

  125. 26:125

    إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

    Innee lakum Rasoolun ameen

    Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

  126. 26:126

    فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

    Fattaqullaaha wa atee'oon

    Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

  127. 26:127

    وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Wa maa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

    Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  128. 26:128

    أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةًۭ تَعْبَثُونَ

    Atabnoona bikulli ree'in aayatan ta'basoon

    Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?

  129. 26:129

    وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ

    Wa tattakhizoona masaani'a la'allakum takhludoon

    Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!

  130. 26:130

    وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ

    Wa izaa batashtum batashtum jabbaareen

    Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.

  131. 26:131

    فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

    Fattaqul laaha wa atee'oon

    Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

  132. 26:132

    وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِىٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ

    Wattaqul lazeee amad dakum bimaa ta'lamoon

    Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.

  133. 26:133

    أَمَدَّكُم بِأَنْعَٰمٍۢ وَبَنِينَ

    Amaddakum bi an'aa minw wa baneen

    Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.

  134. 26:134

    وَجَنَّٰتٍۢ وَعُيُونٍ

    Wa jannaatinw wa 'uyoon

    Na mabustani na chemchem.

  135. 26:135

    إِنِّىٓ أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍۢ

    Innee akhaafu 'alaikum 'azaaba Yawmin 'azeem

    Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.

  136. 26:136

    قَالُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْنَآ أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ ٱلْوَٰعِظِينَ

    Qaaloo sawaaa'un 'alainaaa awa 'azta am lam takum minal waa'izeen

    Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.

  137. 26:137

    إِنْ هَٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلْأَوَّلِينَ

    In haazaaa illaa khuluqul awwaleen

    Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.

  138. 26:138

    وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ

    Wa maa nahnu bimu 'azzabeen

    Wala sisi hatutaadhibiwa.

  139. 26:139

    فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَٰهُمْ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

    Fakazzaboohu fa ahlaknaahum; inna fee zaalika la aayah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

    Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

  140. 26:140

    وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

    Wa inna Rabbaka la huwal 'Azeezur Raheem

    Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

  141. 26:141

    كَذَّبَتْ ثَمُودُ ٱلْمُرْسَلِينَ

    Kazzabat Samoodul mursaleen

    Kina Thamud waliwakanusha Mitume.

  142. 26:142

    إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

    Iz qaala lahum akhoohum Saalihun alaa tattaqoon

    Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?

  143. 26:143

    إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

    Innee lakum Rasoolun ameen

    Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

  144. 26:144

    فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

    Fattaqul laaha wa atee'oon

    Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

  145. 26:145

    وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Wa maaa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

    Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  146. 26:146

    أَتُتْرَكُونَ فِى مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ

    Atutrakoona fee maa haahunnaaa aamineen

    Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?

  147. 26:147

    فِى جَنَّٰتٍۢ وَعُيُونٍۢ

    Fee jannaatinw wa 'uyoon

    Katika mabustani, na chemchem?

  148. 26:148

    وَزُرُوعٍۢ وَنَخْلٍۢ طَلْعُهَا هَضِيمٌۭ

    Wa zuroo inw wa nakhlin tal 'uhaa hadeem

    Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.

  149. 26:149

    وَتَنْحِتُونَ مِنَ ٱلْجِبَالِ بُيُوتًۭا فَٰرِهِينَ

    Wa tanhitoona minal jibaali buyootan faariheen

    Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.

  150. 26:150

    فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

    Fattaqul laaha wa atee'oon

    Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

  151. 26:151

    وَلَا تُطِيعُوٓا۟ أَمْرَ ٱلْمُسْرِفِينَ

    Wa laa tutee'ooo amral musrifeen

    Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,

  152. 26:152

    ٱلَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِى ٱلْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ

    Allazeena yufsidoona fil ardi wa laa yuslihoon

    Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.

  153. 26:153

    قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ

    Qaalooo innamaa anta minal musahhareen

    Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.

  154. 26:154

    مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌۭ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

    Maaa anta illaa basharum mislunaa faati bi Aayatin in kunta minas saadiqeen

    Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

  155. 26:155

    قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٌۭ لَّهَا شِرْبٌۭ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍۢ مَّعْلُومٍۢ

    Qaala haazihee naaqatul lahaa shirbunw w alakum shirbu yawmim ma'loom

    Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.

  156. 26:156

    وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٍۢ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍۢ

    Wa laa tamassoohaa bisooo'in fa yaakhuzakum 'azaabu Yawmin 'Azeem

    Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.

  157. 26:157

    فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا۟ نَٰدِمِينَ

    Fa'aqaroohaa fa asbahoo naadimeen

    Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.

  158. 26:158

    فَأَخَذَهُمُ ٱلْعَذَابُ ۗ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

    Fa akhazahumul 'azaab; inna fee zaalika la Aayah; wa maa kaana aksaruhum m'mineen

    Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

  159. 26:159

    وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

    Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

    Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

  160. 26:160

    كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ ٱلْمُرْسَلِينَ

    kazzabat qawmu Lootinil mursaleen

    Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.

  161. 26:161

    إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ

    Iz qaala lahum akhoohum Lootun alaa tattaqoon

    Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?

  162. 26:162

    إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

    Innee lakum rasoolun ameen

    Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.

  163. 26:163

    فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

    Fattaqul laaha wa atee'oon

    Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.

  164. 26:164

    وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Wa maaa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

    Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  165. 26:165

    أَتَأْتُونَ ٱلذُّكْرَانَ مِنَ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Ataatoonaz zukraana minal 'aalameen

    Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?

  166. 26:166

    وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَٰجِكُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ

    Wa tazaroona maa khalaqa lakum Rabbukum min azwaajikum; bal antum qawmun 'aadoon

    Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!

  167. 26:167

    قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمُخْرَجِينَ

    Qaloo la'il lam tantahi yaa Lootu latakoonanna minal mukhrajeen

    Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!

  168. 26:168

    قَالَ إِنِّى لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلْقَالِينَ

    Qaala innee li'amalikum minal qaaleen

    Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.

  169. 26:169

    رَبِّ نَجِّنِى وَأَهْلِى مِمَّا يَعْمَلُونَ

    Rabbi najjjinee wa ahlee mimmmaa ya'maloon

    Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.

  170. 26:170

    فَنَجَّيْنَٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ

    Fanajjainaahu wa ahlahooo ajma'een

    Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,

  171. 26:171

    إِلَّا عَجُوزًۭا فِى ٱلْغَٰبِرِينَ

    Illaa 'ajoozan filghaabireen

    Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.

  172. 26:172

    ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْءَاخَرِينَ

    Summa dammarnal aa khareen

    Kisha tukawaangamiza wale wengine.

  173. 26:173

    وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًۭا ۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلْمُنذَرِينَ

    Wa amtarnaa 'alaihim mataran fasaaa'a matarul munzareen

    Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.

  174. 26:174

    إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

    Inna fee zaalika la Aayah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

    Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

  175. 26:175

    وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

    Wa inna Rabbaka la Huwal 'Azeezur Raheem

    Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

  176. 26:176

    كَذَّبَ أَصْحَٰبُ لْـَٔيْكَةِ ٱلْمُرْسَلِينَ

    Kazzaba As haabul Aykatil mursaleen

    Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.

  177. 26:177

    إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ

    Iz qaala lahum Shu'aybun alaa tattaqoon

    Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?

  178. 26:178

    إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌۭ

    Innee lakum Rasoolun ameen

    Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

  179. 26:179

    فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

    Fattaqul laaha wa atee'oon

    Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

  180. 26:180

    وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Wa maaa as'alukum 'alaihi min ajrin in ajriya illaa 'alaa Rabbil 'aalameen

    Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  181. 26:181

    ۞ أَوْفُوا۟ ٱلْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا۟ مِنَ ٱلْمُخْسِرِينَ

    Awful kaila wa laa takoonoo minal mukhsireen

    Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.

  182. 26:182

    وَزِنُوا۟ بِٱلْقِسْطَاسِ ٱلْمُسْتَقِيمِ

    Wa zinoo bilqistaasil mustaqeem

    Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;

  183. 26:183

    وَلَا تَبْخَسُوا۟ ٱلنَّاسَ أَشْيَآءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا۟ فِى ٱلْأَرْضِ مُفْسِدِينَ

    Wa laa tabkhasun naasa ashyaaa 'ahum wa laa ta'saw fil ardi mufsideen

    Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.

  184. 26:184

    وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِى خَلَقَكُمْ وَٱلْجِبِلَّةَ ٱلْأَوَّلِينَ

    Wattaqul lazee khalaqakum waljibillatal awwaleen

    Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.

  185. 26:185

    قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ

    Qaalooo innamaa anta minal musahhareen

    Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.

  186. 26:186

    وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌۭ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلْكَٰذِبِينَ

    Wa maaa anta illaa basharum mislunaa wa innazunnuka laminal kaazibeen

    Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.

  187. 26:187

    فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًۭا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

    Fa asqit 'alainaa kisafam minas samaaa'i in kunta minas saadiqeen

    Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

  188. 26:188

    قَالَ رَبِّىٓ أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ

    Qaala Rabbeee a'lamu bimaa ta'maloon

    Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.

  189. 26:189

    فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ ٱلظُّلَّةِ ۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ

    Fakazzaboohu fa akhazahum 'azaabu Yawmiz zullah; innahoo kaana 'azaaba Yawmin 'Azeem

    Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.

  190. 26:190

    إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَءَايَةًۭ ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ

    Inna fee zaalika la Aayah; wa maa kaana aksaruhum mu'mineen

    Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

  191. 26:191

    وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

    Wa inna Rabbaka la huwal 'Azeezur Raheem

    Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

  192. 26:192

    وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

    Wa innahoo latanzeelu Rabbil 'aalameen

    Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

  193. 26:193

    نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلْأَمِينُ

    Nazala bihir Roohul Ameen

    Ameuteremsha Roho muaminifu,

  194. 26:194

    عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلْمُنذِرِينَ

    'Alaa qalbika litakoona minal munzireen

    Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,

  195. 26:195

    بِلِسَانٍ عَرَبِىٍّۢ مُّبِينٍۢ

    Bilisaanin 'Arabiyyim mubeen

    Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.

  196. 26:196

    وَإِنَّهُۥ لَفِى زُبُرِ ٱلْأَوَّلِينَ

    Wa innahoo lafee Zuburil awwaleen

    Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.

  197. 26:197

    أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ ءَايَةً أَن يَعْلَمَهُۥ عُلَمَٰٓؤُا۟ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ

    Awalam yakul lahum Aayatan ai ya'lamahoo 'ulamaaa'u Baneee Israaa'eel

    Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?

  198. 26:198

    وَلَوْ نَزَّلْنَٰهُ عَلَىٰ بَعْضِ ٱلْأَعْجَمِينَ

    Wa law nazzalnaahu 'alaa ba'dil a'jameen

    Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,

  199. 26:199

    فَقَرَأَهُۥ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا۟ بِهِۦ مُؤْمِنِينَ

    Faqara ahoo 'alaihim maa kaanoo bihee mu'mineen

    Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.

  200. 26:200

    كَذَٰلِكَ سَلَكْنَٰهُ فِى قُلُوبِ ٱلْمُجْرِمِينَ

    Kazaalika salaknaahu fee quloobil mujrimeen

    Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.

  201. 26:201

    لَا يُؤْمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُا۟ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ

    Laa yu'minoona bihee hattaa yarawul 'azaabal aleem

    Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.

  202. 26:202

    فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةًۭ وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ

    Fayaatiyahum baghtatanw wa hum laa yash'uroon

    Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.

  203. 26:203

    فَيَقُولُوا۟ هَلْ نَحْنُ مُنظَرُونَ

    Fa yaqooloo hal nahnu munzaroon

    Na watasema: Je, tutapewa muhula?

  204. 26:204

    أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ

    Aafabi 'azaabinaa yasta'jiloon

    Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?

  205. 26:205

    أَفَرَءَيْتَ إِن مَّتَّعْنَٰهُمْ سِنِينَ

    Aara'aita im matta'naahum sineen

    Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,

  206. 26:206

    ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُوا۟ يُوعَدُونَ

    Summa jaaa'ahum maa kaanoo yoo'adoon

    Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,

  207. 26:207

    مَآ أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا۟ يُمَتَّعُونَ

    Maaa aghnaaa 'anhum maa kaanoo yumaatoo'oon

    Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?

  208. 26:208

    وَمَآ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ

    Wa maaa ahlaknaa min qaryatin illaa lahaa munziroon

    Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -

  209. 26:209

    ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

    Zikraa wa maa kunnaa zaalimeen

    Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.

  210. 26:210

    وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ

    Wa maa tanazzalat bihish Shayaateen

    Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,

  211. 26:211

    وَمَا يَنۢبَغِى لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ

    Wa maa yambaghee lahum wa maa yastatee'oon

    Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.

  212. 26:212

    إِنَّهُمْ عَنِ ٱلسَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ

    Innahum 'anis sam'i lama'zooloon

    Hakika hao wametengwa na kusikia.

  213. 26:213

    فَلَا تَدْعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلْمُعَذَّبِينَ

    Falaa tad'u ma'al laahi ilaahan aakhara fatakoona minal mu'azzabeen

    Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.

  214. 26:214

    وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ ٱلْأَقْرَبِينَ

    Wa anzir 'asheeratakal aqrabeen

    Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.

  215. 26:215

    وَٱخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

    Wakhfid janaahaka limanit taba 'aka minal mu'mineen

    Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.

  216. 26:216

    فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّى بَرِىٓءٌۭ مِّمَّا تَعْمَلُونَ

    Fa in asawka faqul innee bareee'um mimmmaa ta'maloon

    Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.

  217. 26:217

    وَتَوَكَّلْ عَلَى ٱلْعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ

    Wa tawakkal alal 'Azeezir Raheem

    Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

  218. 26:218

    ٱلَّذِى يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ

    Allazee yaraaka heena taqoom

    Ambaye anakuona unapo simama,

  219. 26:219

    وَتَقَلُّبَكَ فِى ٱلسَّٰجِدِينَ

    Wa taqallubaka fis saajideen

    Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.

  220. 26:220

    إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ

    Innahoo Huwas Samee'ul 'Aleem

    Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.

  221. 26:221

    هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَٰطِينُ

    Hal unabbi'ukum 'alaa man tanazzalush Shayaateen

    Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?

  222. 26:222

    تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍۢ

    Tanazzalu 'alaa kulli affaakin aseem

    Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.

  223. 26:223

    يُلْقُونَ ٱلسَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَٰذِبُونَ

    Yulqoonas sam'a wa aksaruhum aaziboon

    Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.

  224. 26:224

    وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلْغَاوُۥنَ

    Washshu 'araaa'u yattabi 'uhumul ghaawoon

    Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.

  225. 26:225

    أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِى كُلِّ وَادٍۢ يَهِيمُونَ

    Alam tara annahum fee kulli waadiny yaheemoon

    Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?

  226. 26:226

    وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ

    Wa annahum yaqooloona ma laa yaf'aloon

    Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?

  227. 26:227

    إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَذَكَرُوا۟ ٱللَّهَ كَثِيرًۭا وَٱنتَصَرُوا۟ مِنۢ بَعْدِ مَا ظُلِمُوا۟ ۗ وَسَيَعْلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓا۟ أَىَّ مُنقَلَبٍۢ يَنقَلِبُونَ

    Illal lazeena aamanoo w a'amilus saalihaati wa zakarul laaha kaseeranw wantasaroo mim ba'di maa zulimoo; wa saya'lamul lazeena zalamooo aiya munqalbiny yanqaliboon

    Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.

About Surah Ash-Shu'ara

Ash-Shu'ara, the Poets, recounts the stories of Musa, Ibrahim, Nuh, Hud, Salih, Lut, and Shu'ayb, each calling his people and each met with rejection. The repeated refrain underlines that the messengers asked for no reward and sought only to guide. The surah ends by clearing the Prophet (peace be upon him) of the charge that he was merely a poet.

Themes: Stories of the messengers, Calling people to truth, Rejection and patience, The truth of revelation

Arabic: Uthmani script (Hafs). Translation: Swahili. Recitation: Mishary Rashid Alafasy. See Sources for full attribution.