Surah As-Saffat (undefined) is the 37th chapter of the Holy Quran. It was revealed in Mecca and contains 182 verses (ayahs). Read it below with the Arabic text, transliteration, and Swahili translation, or open it as interactive flashcards to memorize it verse by verse.
- 37:1
وَٱلصَّٰٓفَّٰتِ صَفًّۭا
Wassaaaffaati saffaa
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
- 37:2
فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجْرًۭا
Fazzaajiraati zajraa
Na kwa wenye kukataza mabaya.
- 37:3
فَٱلتَّٰلِيَٰتِ ذِكْرًا
Fattaaliyaati Zikra
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
- 37:4
إِنَّ إِلَٰهَكُمْ لَوَٰحِدٌۭ
Inna Illaahakum la Waahid
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
- 37:5
رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ ٱلْمَشَٰرِقِ
Rabbus samaawaati wal ardi wa maa bainahumaa wa Rabbul mashaariq
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
- 37:6
إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنْيَا بِزِينَةٍ ٱلْكَوَاكِبِ
Innaa zaiyannas samaaa 'ad dunyaa bizeenatinil kawaakib
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
- 37:7
وَحِفْظًۭا مِّن كُلِّ شَيْطَٰنٍۢ مَّارِدٍۢ
Wa hifzam min kulli Shaitaanim maarid
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
- 37:8
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلْمَلَإِ ٱلْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍۢ
Laa yassamma 'oona ilal mala il a'alaa wa yuqzafoona min kulli jaanib
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
- 37:9
دُحُورًۭا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌۭ وَاصِبٌ
Duhooranw wa lahum 'azaabunw waasib
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
- 37:10
إِلَّا مَنْ خَطِفَ ٱلْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌۭ ثَاقِبٌۭ
Illaa man khatifal khatfata fa atba'ahoo shihaabun saaqib
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
- 37:11
فَٱسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَآ ۚ إِنَّا خَلَقْنَٰهُم مِّن طِينٍۢ لَّازِبٍۭ
Fastaftihim ahum ashaddu khalqan am man khalaqnaa; innaa khalaqnaahum min teenil laazib
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
- 37:12
بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ
Bal'ajibta wa yaskharoon
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
- 37:13
وَإِذَا ذُكِّرُوا۟ لَا يَذْكُرُونَ
Wa izaa zukkiroo laa yazkuroon
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
- 37:14
وَإِذَا رَأَوْا۟ ءَايَةًۭ يَسْتَسْخِرُونَ
Wa izaa ra aw Aayatinw yastaskhiroon
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
- 37:15
وَقَالُوٓا۟ إِنْ هَٰذَآ إِلَّا سِحْرٌۭ مُّبِينٌ
Wa qaalooo in haazaa illaa sihrum mubeen
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
- 37:16
أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًۭا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
'A-izaa mitnaa wa kunnaa turaabanw wa 'izaaman 'ainnaa lamab'oosoon
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
- 37:17
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ
Awa aabaa'unal awwaloon
Hata baba zetu wa zamani?
- 37:18
قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَٰخِرُونَ
Qul na'am wa antum daakhiroon
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
- 37:19
فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌۭ وَٰحِدَةٌۭ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ
Fa innamaa hiya zajra tunw waahidatun fa izaa hum yanzuroon
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
- 37:20
وَقَالُوا۟ يَٰوَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Qa qaaloo yaa wailanaa haazaa Yawmud-Deen
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
- 37:21
هَٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Haazaa Yawmul Faslil lazee kuntum bihee tukaziboon
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
- 37:22
۞ ٱحْشُرُوا۟ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ وَأَزْوَٰجَهُمْ وَمَا كَانُوا۟ يَعْبُدُونَ
Uhshurul lazeena zalamoo wa azwaajahum wa maa kaanoo ya'budoon
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
- 37:23
مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلْجَحِيمِ
Min doonil laahi fahdoohum ilaa siraatil Jaheem
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
- 37:24
وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْـُٔولُونَ
Wa qifoohum innahum mas'ooloon
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
- 37:25
مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ
Maa lakum laa tanaasaroon
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
- 37:26
بَلْ هُمُ ٱلْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ
Bal humul Yawma mustaslimoon
Bali hii leo, watasalimu amri.
- 37:27
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍۢ يَتَسَآءَلُونَ
Wa aqbala ba'duhum 'alaa ba'diny yatasaaa'aloon
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
- 37:28
قَالُوٓا۟ إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ ٱلْيَمِينِ
Qaalooo innakum kuntum taatoonanaa 'anil yameen
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
- 37:29
قَالُوا۟ بَل لَّمْ تَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
Qaaloo bal lam takoonoo mu'mineen
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
- 37:30
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَٰنٍۭ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًۭا طَٰغِينَ
Wa maa kaana lanaa 'alaikum min sultaanim bal kuntum qawman taagheen
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
- 37:31
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَآ ۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ
Fahaqqa 'alainaa qawlu Rabbinaaa innaa lazaaa'iqoon
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
- 37:32
فَأَغْوَيْنَٰكُمْ إِنَّا كُنَّا غَٰوِينَ
Fa aghwainaakum innaa kunnaa ghaaween
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
- 37:33
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍۢ فِى ٱلْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ
Fa innahum Yawma'izin fil'azaabi mushtarikoon
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
- 37:34
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ
Innaa kazaalika naf'alu bil mujrimeen
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
- 37:35
إِنَّهُمْ كَانُوٓا۟ إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ
Innahum kaanooo izaa qeela lahum laaa ilaaha illal laahu yastakbiroon
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
- 37:36
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓا۟ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٍۢ مَّجْنُونٍۭ
Wa yaqooloona a'innaa lataarikooo aalihatinaa lishaa'irim majnoon
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
- 37:37
بَلْ جَآءَ بِٱلْحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلْمُرْسَلِينَ
bal jaaa'a bilhaqqi wa saddaqal mursaleen
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
- 37:38
إِنَّكُمْ لَذَآئِقُوا۟ ٱلْعَذَابِ ٱلْأَلِيمِ
Innakum lazaaa'iqul 'azaabil aleem
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
- 37:39
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Wa maa tujzawna illaa maa kuntum ta'maloon
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
- 37:40
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Illaa 'ibaadal laahil mukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
- 37:41
أُو۟لَٰٓئِكَ لَهُمْ رِزْقٌۭ مَّعْلُومٌۭ
Ulaaa'ika lahum rizqum ma'loom
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
- 37:42
فَوَٰكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ
Fa waakihu wa hum mukramoon
Matunda, nao watahishimiwa.
- 37:43
فِى جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Fee jannaatin Na'eem
Katika Bustani za neema.
- 37:44
عَلَىٰ سُرُرٍۢ مُّتَقَٰبِلِينَ
'Alaa sururim mutaqaa bileen
Wako juu ya viti wamekabiliana.
- 37:45
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍۢ مِّن مَّعِينٍۭ
Yutaafu 'alaihim bikaasim mim ma'een
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
- 37:46
بَيْضَآءَ لَذَّةٍۢ لِّلشَّٰرِبِينَ
Baidaaa'a laz zatil lish shaaribeen
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
- 37:47
لَا فِيهَا غَوْلٌۭ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ
Laa feehaa ghawlunw wa laa hum 'anhaa yunzafoon
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
- 37:48
وَعِندَهُمْ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ عِينٌۭ
Wa 'indahum qaasiraatut tarfi 'een
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
- 37:49
كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌۭ مَّكْنُونٌۭ
Ka annahunna baidum maknoon
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
- 37:50
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍۢ يَتَسَآءَلُونَ
Fa aqbala ba'duhum 'alaa badiny yatasaaa 'aloon
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
- 37:51
قَالَ قَآئِلٌۭ مِّنْهُمْ إِنِّى كَانَ لِى قَرِينٌۭ
Qaala qaaa'ilum minhum innee kaana lee qareen
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
- 37:52
يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلْمُصَدِّقِينَ
Yaqoolu a'innnaka laminal musaddiqeen
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
- 37:53
أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًۭا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ
'A-izaa mitnaa wa kunnaa turaabanw wa 'izaaman 'ainnaa lamadeenoon
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
- 37:54
قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Qaala hal antum muttali'oon
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
- 37:55
فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِى سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ
Fattala'a fara aahu fee sawaaa'il Jaheem
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
- 37:56
قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ
Qaala tallaahi in kitta laturdeen
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
- 37:57
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّى لَكُنتُ مِنَ ٱلْمُحْضَرِينَ
Wa law laa ni'matu Rabbee lakuntu minal muhdareen
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
- 37:58
أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ
Afamaa nahnu bimaiyiteen
Je! Sisi hatutakufa,
- 37:59
إِلَّا مَوْتَتَنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Illa mawtatanal oola wa maa nahnu bimu'azzabeen
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
- 37:60
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ
Inna haazaa falya'ma lil'aamiloon
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
- 37:61
لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ ٱلْعَٰمِلُونَ
Limisli haaza falya'ma lil 'aamiloon
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
- 37:62
أَذَٰلِكَ خَيْرٌۭ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ
Azaalika khairun nuzulan am shajaratuz Zaqqom
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
- 37:63
إِنَّا جَعَلْنَٰهَا فِتْنَةًۭ لِّلظَّٰلِمِينَ
Innaa ja'alnaahaa fitnatal lizzaalimeen
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
- 37:64
إِنَّهَا شَجَرَةٌۭ تَخْرُجُ فِىٓ أَصْلِ ٱلْجَحِيمِ
Innahaa shajaratun takhruju feee aslil Jaheem
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
- 37:65
طَلْعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَٰطِينِ
Tal'uhaa ka annahoo ru'oosush Shayaateen
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
- 37:66
فَإِنَّهُمْ لَءَاكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ
Fa innahum la aakiloona minhaa famaali'oona minhal butoon
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
- 37:67
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًۭا مِّنْ حَمِيمٍۢ
Summa inna lahum 'alaihaa lashawbam min hameem
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
- 37:68
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى ٱلْجَحِيمِ
Summa inna marji'ahum la ilal Jaheem
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
- 37:69
إِنَّهُمْ أَلْفَوْا۟ ءَابَآءَهُمْ ضَآلِّينَ
Innahum alfaw aabaaa'ahum daaalleen
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
- 37:70
فَهُمْ عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِمْ يُهْرَعُونَ
Fahum 'alaa aasaarihim yuhra'oon
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
- 37:71
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ ٱلْأَوَّلِينَ
Wa laqad dalla qablahum aksarul awwaleen
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
- 37:72
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Wa laqad arsalnaa feehim munzireen
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
- 37:73
فَٱنظُرْ كَيْفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلْمُنذَرِينَ
Fanzur kaifa kaana 'aaqibatul munzareen
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
- 37:74
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Illaa 'ibaadal laahil mukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
- 37:75
وَلَقَدْ نَادَىٰنَا نُوحٌۭ فَلَنِعْمَ ٱلْمُجِيبُونَ
Wa laqad naadaanaa Noohun falani'mal mujeeboon
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
- 37:76
وَنَجَّيْنَٰهُ وَأَهْلَهُۥ مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
Wa jajainaahu wa ahlahoo minal karbil 'azeem
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
- 37:77
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلْبَاقِينَ
Wa ja'alnaa zurriyyatahoo hummul baaqeen
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
- 37:78
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْءَاخِرِينَ
Wa taraknaa 'alaihi fil aakhireen
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
- 37:79
سَلَٰمٌ عَلَىٰ نُوحٍۢ فِى ٱلْعَٰلَمِينَ
Salaamun 'alaa Noohin fil 'aalameen
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
- 37:80
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Innaa kazaalika najzil muhsineen
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
- 37:81
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Innahoo min 'ibaadinal mu'mineen
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
- 37:82
ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْءَاخَرِينَ
Summa aghraqnal aakhareen
Kisha tukawazamisha wale wengine.
- 37:83
۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبْرَٰهِيمَ
Wa ina min shee'atihee la Ibraaheem
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
- 37:84
إِذْ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلْبٍۢ سَلِيمٍ
Iz jaaa'a Rabbahoo bi qalbin saleem
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
- 37:85
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَاذَا تَعْبُدُونَ
Iz qaala li abeehi wa qawmihee maazaa ta'budoon
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
- 37:86
أَئِفْكًا ءَالِهَةًۭ دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ
A'ifkan aalihatan doonal laahi tureedoon
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
- 37:87
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Famaa zannukum bi Rabbil'aalameen
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
- 37:88
فَنَظَرَ نَظْرَةًۭ فِى ٱلنُّجُومِ
Fanazara nazratan finnujoom
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
- 37:89
فَقَالَ إِنِّى سَقِيمٌۭ
Faqaala inee saqeem
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
- 37:90
فَتَوَلَّوْا۟ عَنْهُ مُدْبِرِينَ
Fatawallaw 'anhu mudbireen
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
- 37:91
فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Faraagha ilaaa aalihatihim faqaala alaa taakuloon
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
- 37:92
مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ
Maa lakum laa tantiqoon
Mna nini hata hamsemi?
- 37:93
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًۢا بِٱلْيَمِينِ
Faraagha 'alaihim darbam bilyameen
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
- 37:94
فَأَقْبَلُوٓا۟ إِلَيْهِ يَزِفُّونَ
Fa aqbalooo ilaihi yaziffoon
Basi wakamjia upesi upesi.
- 37:95
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ
Qaala ata'budoona maa tanhitoon
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
- 37:96
وَٱللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
Wallaahu khalaqakum wa maa ta'maloon
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
- 37:97
قَالُوا۟ ٱبْنُوا۟ لَهُۥ بُنْيَٰنًۭا فَأَلْقُوهُ فِى ٱلْجَحِيمِ
Qaalub noo lahoo bun yaanan fa alqoohu fil jaheem
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
- 37:98
فَأَرَادُوا۟ بِهِۦ كَيْدًۭا فَجَعَلْنَٰهُمُ ٱلْأَسْفَلِينَ
Fa araadoo bihee kaidan faja 'alnaahumul asfaleen
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
- 37:99
وَقَالَ إِنِّى ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّى سَيَهْدِينِ
Wa qaala innee zaahibun ilaa Rabbee sa yahdeen
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
- 37:100
رَبِّ هَبْ لِى مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Rabbi hab lee minas saaliheen
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
- 37:101
فَبَشَّرْنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٍۢ
Fabashsharnaahu bighulaamin haleem
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
- 37:102
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعْىَ قَالَ يَٰبُنَىَّ إِنِّىٓ أَرَىٰ فِى ٱلْمَنَامِ أَنِّىٓ أَذْبَحُكَ فَٱنظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَٰٓأَبَتِ ٱفْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِىٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّٰبِرِينَ
Falamma balagha ma'a hus sa'ya qaala yaa buniya inneee araa fil manaami anneee azbahuka fanzur maazaa taraa; qaala yaaa abatif 'al maa tu'maru satajidunee in shaaa'allaahu minas saabireen
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
- 37:103
فَلَمَّآ أَسْلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلْجَبِينِ
Falammaaa aslamaa wa tallahoo liljabeen
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
- 37:104
وَنَٰدَيْنَٰهُ أَن يَٰٓإِبْرَٰهِيمُ
Wa naadainaahu ai yaaaa Ibraheem
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
- 37:105
قَدْ صَدَّقْتَ ٱلرُّءْيَآ ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Qad saddaqtar ru'yaa; innaa kazaalika najzil muhsineen
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
- 37:106
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلْبَلَٰٓؤُا۟ ٱلْمُبِينُ
Inna haazaa lahuwal balaaa'ul mubeen
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
- 37:107
وَفَدَيْنَٰهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍۢ
Wa fadainaahu bizibhin 'azeem
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
- 37:108
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْءَاخِرِينَ
Wa taraknaa 'alaihi fil aakhireen
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
- 37:109
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبْرَٰهِيمَ
Salaamun 'alaaa Ibraaheem
Iwe salama kwa Ibrahim!
- 37:110
كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Kazaalika najzil muhsineen
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
- 37:111
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Innahoo min 'ibaadinal mu'mineen
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
- 37:112
وَبَشَّرْنَٰهُ بِإِسْحَٰقَ نَبِيًّۭا مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Wa bashsharnaahu bi Ishaaqa Nabiyayam minas saaliheen
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
- 37:113
وَبَٰرَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰٓ إِسْحَٰقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌۭ وَظَالِمٌۭ لِّنَفْسِهِۦ مُبِينٌۭ
Wa baaraknaa 'alaihi wa 'alaaa Ishaaq; wa min zurriyya tihimaa muhsinunw wa zaalimul linafshihee mubeen
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
- 37:114
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Wa laqad mananna alaa Moosaa wa Haaroon
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
- 37:115
وَنَجَّيْنَٰهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
Wa najjainaahumaa wa qawmahumaa minal karbil 'azeem
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
- 37:116
وَنَصَرْنَٰهُمْ فَكَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَٰلِبِينَ
Wa nasarnaahum fakaanoo humul ghaalibeen
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
- 37:117
وَءَاتَيْنَٰهُمَا ٱلْكِتَٰبَ ٱلْمُسْتَبِينَ
Wa aatainaahumal Kitaabal mustabeen
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
- 37:118
وَهَدَيْنَٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ
Wa hadainaahumus Siraatal Mustaqeem
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
- 37:119
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِى ٱلْءَاخِرِينَ
Wa taraknaa 'alaihimaa fil aakhireen
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
- 37:120
سَلَٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Salaamun 'alaa Moosaa wa Haaroon
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
- 37:121
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Innaa kazaalika najzil muhsineen
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
- 37:122
إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Innahumaa min 'ibaadinal mu'mineen
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
- 37:123
وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Wa inna Ilyaasa laminal mursaleen
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
- 37:124
إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ
Iz qaala liqawmiheee alaa tattaqoon
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
- 37:125
أَتَدْعُونَ بَعْلًۭا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ ٱلْخَٰلِقِينَ
Atad'oona Ba'lanw wa tazaroona ahsanal khaaliqeen
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
- 37:126
ٱللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
Allaaha Rabbakum wa Rabba aabaaa'ikumul awwaleen
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
- 37:127
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
Fakazzaboohu fa inna hum lamuhdaroon
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
- 37:128
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Illaa 'ibaadal laahil mukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
- 37:129
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْءَاخِرِينَ
Wa taraknaa 'alaihi fil aakhireen
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
- 37:130
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلْ يَاسِينَ
Salaamun 'alaaa Ilyaaseen
Iwe salama kwa Ilyas.
- 37:131
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Innaa kazaalika najzil muhsineen
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
- 37:132
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Innahoo min 'ibaadinal mu'mineen
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
- 37:133
وَإِنَّ لُوطًۭا لَّمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Wa inna Lootal laminal mursaleen
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
- 37:134
إِذْ نَجَّيْنَٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
Iz najjainaahu wa ahlahooo ajma'een
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
- 37:135
إِلَّا عَجُوزًۭا فِى ٱلْغَٰبِرِينَ
Illaa 'ajoozan fil ghaabireen
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
- 37:136
ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْءَاخَرِينَ
Summa dammarnal aakhareen
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
- 37:137
وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ
Wa innakum latamurroona 'alaihim musbiheen
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
- 37:138
وَبِٱلَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
Wa billail; afalaa ta'qiloon
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
- 37:139
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Wa inna Yoonusa laminal mursaleen
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
- 37:140
إِذْ أَبَقَ إِلَى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
Iz abaqa ilal fulkil mash hoon
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
- 37:141
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلْمُدْحَضِينَ
Fasaahama fakaana minal mudhadeen
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
- 37:142
فَٱلْتَقَمَهُ ٱلْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌۭ
Faltaqamahul hootu wa huwa muleem
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
- 37:143
فَلَوْلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلْمُسَبِّحِينَ
Falaw laaa annahoo kaana minal musabbiheen
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
- 37:144
لَلَبِثَ فِى بَطْنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
Lalabisa fee batniheee ilaa Yawmi yub'asoon
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
- 37:145
۞ فَنَبَذْنَٰهُ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٌۭ
Fanabaznaahu bil'araaa'i wa huwa saqeem
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
- 37:146
وَأَنۢبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةًۭ مِّن يَقْطِينٍۢ
Wa ambatnaa 'alaihi shajaratam mai yaqteen
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
- 37:147
وَأَرْسَلْنَٰهُ إِلَىٰ مِا۟ئَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ
Wa arsalnaahu ilaa mi'ati alfin aw yazeedoon
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
- 37:148
فَـَٔامَنُوا۟ فَمَتَّعْنَٰهُمْ إِلَىٰ حِينٍۢ
Fa aamanoo famatta' naahum ilaa heen
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
- 37:149
فَٱسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ ٱلْبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلْبَنُونَ
Fastaftihim ali Rabbikal banaatu wa lahumul banoon
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
- 37:150
أَمْ خَلَقْنَا ٱلْمَلَٰٓئِكَةَ إِنَٰثًۭا وَهُمْ شَٰهِدُونَ
Am khalaqnal malaaa'i kata inaasanw wa hm shaahidoon
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
- 37:151
أَلَآ إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ
Alaaa innahum min ifkihim la yaqooloon
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
- 37:152
وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَٰذِبُونَ
Waladal laahu wa innhum lakaaziboon
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
- 37:153
أَصْطَفَى ٱلْبَنَاتِ عَلَى ٱلْبَنِينَ
Astafal banaati 'alal baneen
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
- 37:154
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
Maa lakum kaifa tahkumoon
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
- 37:155
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
Afalaa tazakkaroon
Hamkumbuki?
- 37:156
أَمْ لَكُمْ سُلْطَٰنٌۭ مُّبِينٌۭ
Am lakum sultaanum mubeen
Au mnayo hoja iliyo wazi?
- 37:157
فَأْتُوا۟ بِكِتَٰبِكُمْ إِن كُنتُمْ صَٰدِقِينَ
Faatoo bi Kitaabikum in kuntum saadiqeen
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
- 37:158
وَجَعَلُوا۟ بَيْنَهُۥ وَبَيْنَ ٱلْجِنَّةِ نَسَبًۭا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ ٱلْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
Wa ja'aloo bainahoo wa bainal jinnati nasabaa; wa laqad 'alimatil jinnatu innahum lamuhdaroon
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
- 37:159
سُبْحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
Subhaanal laahi 'ammaa yasifoon
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
- 37:160
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Illaa 'ibaadal laahil mukhlaseen
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
- 37:161
فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ
Fa innakum wa maa ta'ubdoon
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
- 37:162
مَآ أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَٰتِنِينَ
Maaa antum 'alaihi befaaatineen
Hamwezi kuwapoteza
- 37:163
إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ ٱلْجَحِيمِ
Illaa man huwa saalil jaheem
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
- 37:164
وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٌۭ مَّعْلُومٌۭ
Wa maa minnasa illaa lahoo maqaamum ma'loom
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
- 37:165
وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلصَّآفُّونَ
Wa innaa llanah nus saaffoon
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
- 37:166
وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلْمُسَبِّحُونَ
Wa innaa lanah nul musabbihoon
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
- 37:167
وَإِن كَانُوا۟ لَيَقُولُونَ
Wa in kaanoo la yaqooloon
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
- 37:168
لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًۭا مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
Law anna 'indana zikram minal awwaleen
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
- 37:169
لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Lakunna 'ibaadal laahil mukhlaseen
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
- 37:170
فَكَفَرُوا۟ بِهِۦ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Fakafaroo bihee fasawfa ya'lamoon
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
- 37:171
وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلْمُرْسَلِينَ
Wa laqad sabaqat Kalimatunaa li'ibaadinal mursa leen
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
- 37:172
إِنَّهُمْ لَهُمُ ٱلْمَنصُورُونَ
Innaa hum lahumul mansooroon
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
- 37:173
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلْغَٰلِبُونَ
Wa inna jundana lahumul ghaaliboon
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
- 37:174
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍۢ
Fatawalla 'anhum hatta heen
Basi waachilie mbali kwa muda.
- 37:175
وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Wa absirhum fasawfa yubsiroon
Na watazame, nao wataona.
- 37:176
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
Afabi'azaabinaa yasta'jiloon
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
- 37:177
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلْمُنذَرِينَ
Fa izaa nazala bisaahatihim fasaaa'a sabaahul munzareen
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
- 37:178
وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍۢ
Wa tawalla 'anhum hattaa heen
Na waache kwa muda.
- 37:179
وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Wa absir fasawfa yubsiroon
Na tazama, na wao wataona.
- 37:180
سُبْحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
Subhaana Rabbika Rabbil 'izzati 'amma yasifoon
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
- 37:181
وَسَلَٰمٌ عَلَى ٱلْمُرْسَلِينَ
Wa salaamun 'alalmursaleen
Na Salamu juu ya Mitume.
- 37:182
وَٱلْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Walhamdu lillaahi Rabbil 'aalameen
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
About Surah As-Saffat
As-Saffat, Those Who Set the Ranks, opens with the angels arrayed in rows in worship. It recounts the trials of several prophets, most movingly Ibrahim and his readiness to sacrifice his son, and the rescue that followed. It also recalls Nuh, Musa, Ilyas, Lut, and Yunus, drawing a line of devotion through all of them.
Themes: The angels in worship, Ibrahim's sacrifice, Lives of the prophets, Devotion
Arabic: Uthmani script (Hafs). Translation: Swahili. Recitation: Mishary Rashid Alafasy. See Sources for full attribution.