Surah Al-Qamar (undefined) is the 54th chapter of the Holy Quran. It was revealed in Mecca and contains 55 verses (ayahs). Read it below with the Arabic text, transliteration, and Swahili translation, or open it as interactive flashcards to memorize it verse by verse.
- 54:1
ٱقْتَرَبَتِ ٱلسَّاعَةُ وَٱنشَقَّ ٱلْقَمَرُ
Iqtarabatis Saa'atu wsan shaqqal qamar
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
- 54:2
وَإِن يَرَوْا۟ ءَايَةًۭ يُعْرِضُوا۟ وَيَقُولُوا۟ سِحْرٌۭ مُّسْتَمِرٌّۭ
Wa iny yaraw aayatany yu'ridoo wa yaqooloo sihrum mustamirr
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
- 54:3
وَكَذَّبُوا۟ وَٱتَّبَعُوٓا۟ أَهْوَآءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍۢ مُّسْتَقِرٌّۭ
Wa kazzaboo wattaba'ooo ahwaaa'ahum; wa kullu amrim mustaqirr
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
- 54:4
وَلَقَدْ جَآءَهُم مِّنَ ٱلْأَنۢبَآءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ
Wa laqad jaaa'ahum minal ambaaa'i maa feehi muzdajar
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
- 54:5
حِكْمَةٌۢ بَٰلِغَةٌۭ ۖ فَمَا تُغْنِ ٱلنُّذُرُ
Hikmatum baalighatun famaa tughnin nuzur
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
- 54:6
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ ٱلدَّاعِ إِلَىٰ شَىْءٍۢ نُّكُرٍ
Fatawalla 'anhum; yawma yad'ud daa'i ilaa shai 'in nukur
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
- 54:7
خُشَّعًا أَبْصَٰرُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌۭ مُّنتَشِرٌۭ
khushsha'an absaaruhum yakrujoona minal ajdaasi ka annahum jaraadum muntashir
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
- 54:8
مُّهْطِعِينَ إِلَى ٱلدَّاعِ ۖ يَقُولُ ٱلْكَٰفِرُونَ هَٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌۭ
Muhti'eena ilad daa'i yaqoolul kafiroona haazaa yawmun 'asir
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
- 54:9
۞ كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍۢ فَكَذَّبُوا۟ عَبْدَنَا وَقَالُوا۟ مَجْنُونٌۭ وَٱزْدُجِرَ
Kazzabat qablahum qawmu Noohin fakazzaboo 'abdanaa wa qaaloo majnoo nunw wazdujir
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
- 54:10
فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنِّى مَغْلُوبٌۭ فَٱنتَصِرْ
Fada'aa Rabbahooo annee maghloobun fantasir
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
- 54:11
فَفَتَحْنَآ أَبْوَٰبَ ٱلسَّمَآءِ بِمَآءٍۢ مُّنْهَمِرٍۢ
Fafatahnaaa abwaabas sa maaa'i bimaa'im munhamir
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
- 54:12
وَفَجَّرْنَا ٱلْأَرْضَ عُيُونًۭا فَٱلْتَقَى ٱلْمَآءُ عَلَىٰٓ أَمْرٍۢ قَدْ قُدِرَ
Wa fajjamal arda 'uyoonan faltaqal maaa'u 'alaaa amrin qad qudir
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
- 54:13
وَحَمَلْنَٰهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَٰحٍۢ وَدُسُرٍۢ
Wa hamalnaahu 'alaa zaati alwaahinw wa dusur
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
- 54:14
تَجْرِى بِأَعْيُنِنَا جَزَآءًۭ لِّمَن كَانَ كُفِرَ
Tajree bi a'yuninaa jazaaa 'al liman kaana kufir
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
- 54:15
وَلَقَد تَّرَكْنَٰهَآ ءَايَةًۭ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ
Wa laqat taraknaahaad aayatan fahal mim muddakir
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
- 54:16
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
Fakaifa kaana 'azaabee wa nuzur
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
- 54:17
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ
Wa laqad yassamal Quraana liz zikri fahal mimmuddakir
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
- 54:18
كَذَّبَتْ عَادٌۭ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
Kazzabat 'Aadun fakaifa kaana 'azaabee wa nuzur
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
- 54:19
إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًۭا صَرْصَرًۭا فِى يَوْمِ نَحْسٍۢ مُّسْتَمِرٍّۢ
Innaa arsalnaa 'alaihim reehan sarsaran fee Yawmi nahsim mustamirr
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
- 54:20
تَنزِعُ ٱلنَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍۢ مُّنقَعِرٍۢ
Tanzi;un naasa ka anna huma'jaazu nakhlim munqa'ir
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
- 54:21
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
'Fakaifa kaana 'azaabee wa nuzur
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
- 54:22
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ
Wa laqad yassamal Quraana liz zikri fahal mim muddakir
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
- 54:23
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ
Kazzabat Samoodu binnuzur
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
- 54:24
فَقَالُوٓا۟ أَبَشَرًۭا مِّنَّا وَٰحِدًۭا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذًۭا لَّفِى ضَلَٰلٍۢ وَسُعُرٍ
Faqaalooo a-basharam minnaa waahidan nattabi'uhooo innaa izal lafee dalaalinw wa su'ur
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
- 54:25
أَءُلْقِىَ ٱلذِّكْرُ عَلَيْهِ مِنۢ بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌۭ
'A-ulqiyaz zikru 'alaihi mim baininaa bal huwa kazzaabun ashir
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
- 54:26
سَيَعْلَمُونَ غَدًۭا مَّنِ ٱلْكَذَّابُ ٱلْأَشِرُ
Sa-ya'lamoona ghadam manil kazzaabul ashir
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
- 54:27
إِنَّا مُرْسِلُوا۟ ٱلنَّاقَةِ فِتْنَةًۭ لَّهُمْ فَٱرْتَقِبْهُمْ وَٱصْطَبِرْ
Innaa mursilun naaqati fitnatal lahum fartaqibhum wastabir
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
- 54:28
وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ ٱلْمَآءَ قِسْمَةٌۢ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍۢ مُّحْتَضَرٌۭ
Wa nabbi'hum annal maaa'a qismatum bainahum kullu shirbim muhtadar
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
- 54:29
فَنَادَوْا۟ صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ
Fanaadaw saahibahum fata'aataa fa'aqar
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
- 54:30
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
Fakaifa kaana 'azaabee wa nuzur
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
- 54:31
إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةًۭ وَٰحِدَةًۭ فَكَانُوا۟ كَهَشِيمِ ٱلْمُحْتَظِرِ
Innaaa arsalnaa 'alaihim saihatanw waahidatan fakaano kahasheemil muhtazir
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
- 54:32
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ
Wa laqad yassarnal quraana liz zikri fahal mim muddakir
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
- 54:33
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍۭ بِٱلنُّذُرِ
Kazzabat qawmu lootim binnuzur
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
- 54:34
إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّآ ءَالَ لُوطٍۢ ۖ نَّجَّيْنَٰهُم بِسَحَرٍۢ
Innaa arsalnaa 'alaihim haasiban illaaa aala Loot najjainaahum bisahar
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
- 54:35
نِّعْمَةًۭ مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِى مَن شَكَرَ
Ni'matam min 'indinaa; kazaalika najzee man shakar
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
- 54:36
وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا۟ بِٱلنُّذُرِ
Wa laqad anzarahum batshatanaa fatamaaraw binnuzur
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
- 54:37
وَلَقَدْ رَٰوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِۦ فَطَمَسْنَآ أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ
Wa laqad raawadoohu 'andaifee fatamasnaaa a'yunahum fazooqoo 'azaabee wa nuzur
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!
- 54:38
وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌۭ مُّسْتَقِرٌّۭ
Wa laqad sabbahahum bukratan 'azaabum mustaqirr
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
- 54:39
فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ
Fazooqoo 'azaabee wa nuzur
Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
- 54:40
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ
Wa laqad yassarnal Quraana liz zikri fahal mim muddakir
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
- 54:41
وَلَقَدْ جَآءَ ءَالَ فِرْعَوْنَ ٱلنُّذُرُ
Wa laqad jaaa'a Aala Fir'awnan nuzur
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
- 54:42
كَذَّبُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَٰهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍۢ مُّقْتَدِرٍ
Kazzaboo bi Aayaatinaa kullihaa fa akhaznaahum akhza 'azeezim muqtadir
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.
- 54:43
أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌۭ مِّنْ أُو۟لَٰٓئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَآءَةٌۭ فِى ٱلزُّبُرِ
Akuffaarukum khairum min ulaaa'ikum am lakum baraaa'atun fiz Zubur
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
- 54:44
أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌۭ مُّنتَصِرٌۭ
Am yaqooloona nahnu jamee'um muntasir
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
- 54:45
سَيُهْزَمُ ٱلْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ ٱلدُّبُرَ
Sa yuhzamul jam'u wa yuwalloonad dubur
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
- 54:46
بَلِ ٱلسَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَٱلسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ
Balis Saa'atu maw'iduhum was Saa'atu adhaa wa amarr
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
- 54:47
إِنَّ ٱلْمُجْرِمِينَ فِى ضَلَٰلٍۢ وَسُعُرٍۢ
Innal mujrimeena fee dalaalinw wa su'ur
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
- 54:48
يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِى ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا۟ مَسَّ سَقَرَ
Yawma yushaboona fin Naari'alaa wujoohimim zooqoo massa saqar
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
- 54:49
إِنَّا كُلَّ شَىْءٍ خَلَقْنَٰهُ بِقَدَرٍۢ
Innaa kulla shai'in khalaqnaahu biqadar
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
- 54:50
وَمَآ أَمْرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٌۭ كَلَمْحٍۭ بِٱلْبَصَرِ
Wa maaa amrunaaa illaa waahidatun kalamhim bilbasar
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
- 54:51
وَلَقَدْ أَهْلَكْنَآ أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍۢ
Wa laqad ahlaknaaa ashyaa'akum fahal mim muddakir
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
- 54:52
وَكُلُّ شَىْءٍۢ فَعَلُوهُ فِى ٱلزُّبُرِ
Wa kullu shai'in fa'aloohu fiz Zubur
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
- 54:53
وَكُلُّ صَغِيرٍۢ وَكَبِيرٍۢ مُّسْتَطَرٌ
Wa kullu sagheerinw wa kabeerim mustatar
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
- 54:54
إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّٰتٍۢ وَنَهَرٍۢ
Innal muttaqeena fee jannaatinw wa nahar
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
- 54:55
فِى مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍۢ مُّقْتَدِرٍۭ
Fee maq'adi sidqin 'inda Maleekim Muqtadir
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
About Surah Al-Qamar
Al-Qamar, the Moon, opens with the splitting of the moon as a sign and repeats a striking refrain: that Allah has made the Quran easy to remember, so is there anyone who will take heed. It recalls the nations of Nuh, 'Ad, Thamud, Lut, and Pharaoh, each warned and each accountable. The rhythm makes it memorable and sobering.
Themes: The splitting of the moon, The Quran made easy, Past nations, Taking heed
Arabic: Uthmani script (Hafs). Translation: Swahili. Recitation: Mishary Rashid Alafasy. See Sources for full attribution.