Surah Al-Qalam (undefined) is the 68th chapter of the Holy Quran. It was revealed in Mecca and contains 52 verses (ayahs). Read it below with the Arabic text, transliteration, and Swahili translation, or open it as interactive flashcards to memorize it verse by verse.
- 68:1
نٓ ۚ وَٱلْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ
Noon; walqalami wa maa yasturoon
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
- 68:2
مَآ أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍۢ
Maa anta bini'mati Rabbika bimajnoon
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
- 68:3
وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍۢ
Wa inna laka la ajran ghaira mamnoon
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
- 68:4
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍۢ
Wa innaka la'alaa khuluqin 'azeem
Na hakika wewe una tabia tukufu.
- 68:5
فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ
Fasatubsiru wa yubsiroon
Karibu utaona, na wao wataona,
- 68:6
بِأَييِّكُمُ ٱلْمَفْتُونُ
Bi ayyikumul maftoon
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
- 68:7
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعْلَمُ بِٱلْمُهْتَدِينَ
Innaa Rabbaka Huwa a'lamu biman dalla 'an sabeelihee wa Huwa a'lamu bilmuhtadeen
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
- 68:8
فَلَا تُطِعِ ٱلْمُكَذِّبِينَ
Falaa tuti'il mukazzibeen
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
- 68:9
وَدُّوا۟ لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ
Waddoo law tudhinu fa-yudhinoon
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
- 68:10
وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍۢ مَّهِينٍ
Wa laa tuti' kulla hallaa fim maheen
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
- 68:11
هَمَّازٍۢ مَّشَّآءٍۭ بِنَمِيمٍۢ
Hammaazim mash shaaa'im binameem
Mtapitapi, apitaye akifitini,
- 68:12
مَّنَّاعٍۢ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
Mannaa'il lilkhairi mu'tadin aseem
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
- 68:13
عُتُلٍّۭ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
'Utullim ba'da zaalika zaneem
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
- 68:14
أَن كَانَ ذَا مَالٍۢ وَبَنِينَ
An kaana zaa maalinw-wa baneen
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
- 68:15
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ
Izaa tutlaa 'alaihi aayaatunaa qaala asaateerul awwaleen
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
- 68:16
سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلْخُرْطُومِ
Sanasimuhoo 'alal khurtoom
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
- 68:17
إِنَّا بَلَوْنَٰهُمْ كَمَا بَلَوْنَآ أَصْحَٰبَ ٱلْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا۟ لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ
Innaa balawnaahum kamaa balawnaaa As-haabal jannati iz 'aqsamoo la-yasri munnahaa musbiheen
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
- 68:18
وَلَا يَسْتَثْنُونَ
Wa laa yastasnoon
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
- 68:19
فَطَافَ عَلَيْهَا طَآئِفٌۭ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَآئِمُونَ
Fataafa 'alaihaa taaa'i fum mir rabbika wa hum naaa'imoon
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
- 68:20
فَأَصْبَحَتْ كَٱلصَّرِيمِ
Fa asbahat kassareem
Likawa kama usiku wa giza.
- 68:21
فَتَنَادَوْا۟ مُصْبِحِينَ
Fatanaadaw musbiheen
Asubuhi wakaitana.
- 68:22
أَنِ ٱغْدُوا۟ عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَٰرِمِينَ
Anighdoo 'alaa harsikum in kuntum saarimeen
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
- 68:23
فَٱنطَلَقُوا۟ وَهُمْ يَتَخَٰفَتُونَ
Fantalaqoo wa hum yatakhaafatoon
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
- 68:24
أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا ٱلْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌۭ
Al laa yadkhulannahal yawma 'alaikum miskeen
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
- 68:25
وَغَدَوْا۟ عَلَىٰ حَرْدٍۢ قَٰدِرِينَ
Wa ghadaw 'alaa hardin qaadireen
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
- 68:26
فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوٓا۟ إِنَّا لَضَآلُّونَ
Falammaa ra awhaa qaalooo innaa ladaaalloon
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
- 68:27
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
Bal nahnu mahroomoon
Bali tumenyimwa!
- 68:28
قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ
Qaala awsatuhum alam aqul lakum law laa tusabbihoon
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
- 68:29
قَالُوا۟ سُبْحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Qaaloo subhaana rabbinaaa innaa kunnaa zaalimeen
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
- 68:30
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍۢ يَتَلَٰوَمُونَ
Fa aqbala ba'duhum 'alaa ba'diny yatalaawamoon
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
- 68:31
قَالُوا۟ يَٰوَيْلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ
Qaaloo yaa wailanaaa innaa kunnaa taagheen
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
- 68:32
عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًۭا مِّنْهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ
'Asaa rabbunaaa any yubdilanaa khairam minhaaa innaaa ilaa rabbinaa raaghiboon
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
- 68:33
كَذَٰلِكَ ٱلْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ ٱلْءَاخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا۟ يَعْلَمُونَ
Kazaalikal azaab, wa la'azaabul aakhirati akbar; law kaanoo ya'lamoon
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
- 68:34
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Inna lilmuttaqeena 'inda rabbihim jannaatin na'eem
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
- 68:35
أَفَنَجْعَلُ ٱلْمُسْلِمِينَ كَٱلْمُجْرِمِينَ
Afanaj'alul muslimeena kalmujrimeen
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
- 68:36
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
Maa lakum kaifa tahhkumoon
Mna nini? Mnahukumu vipi?
- 68:37
أَمْ لَكُمْ كِتَٰبٌۭ فِيهِ تَدْرُسُونَ
Am lakum kitaabun feehi tadrusoon
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
- 68:38
إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Inna lakum feehi lamaa takhaiyaroon
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
- 68:39
أَمْ لَكُمْ أَيْمَٰنٌ عَلَيْنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ ٱلْقِيَٰمَةِ ۙ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ
Am lakum aymaanun 'alainaa baalighatun ilaa yawmil qiyaamati inna lakum lamaa tahkumoon
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
- 68:40
سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Salhum ayyuhum bizaa lika za'eem
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
- 68:41
أَمْ لَهُمْ شُرَكَآءُ فَلْيَأْتُوا۟ بِشُرَكَآئِهِمْ إِن كَانُوا۟ صَٰدِقِينَ
Am lahum shurakaaa'u falyaatoo bishurakaaa 'ihim in kaanoo saadiqeen
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
- 68:42
يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍۢ وَيُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ
Yawma yukshafu 'am saaqinw wa yud'awna ilas sujoodi falaa yastatee'oon
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
- 68:43
خَٰشِعَةً أَبْصَٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌۭ ۖ وَقَدْ كَانُوا۟ يُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمْ سَٰلِمُونَ
Khaashi'atan absaaruhum tarhaquhum zillatunw wa qad kaanoo yud'awna ilassujoodi wa hum saalimoon
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
- 68:44
فَذَرْنِى وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ
Fazarnee wa many yukazzibu bihaazal hadeesi sanastad rijuhum min haisu laa ya'lamoon
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
- 68:45
وَأُمْلِى لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِى مَتِينٌ
Wa umlee lahum; inna kaidee mateen
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
- 68:46
أَمْ تَسْـَٔلُهُمْ أَجْرًۭا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍۢ مُّثْقَلُونَ
Am tas'aluhum ajran fahum mim maghramim musqaloon
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
- 68:47
أَمْ عِندَهُمُ ٱلْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ
Am 'indahumul ghaibu fahum yaktuboon
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
- 68:48
فَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌۭ
Fasbir lihkmi rabbika wa laa takun kasaahibil boot; iz naadaa wa huwa makzoom
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
- 68:49
لَّوْلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعْمَةٌۭ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ مَذْمُومٌۭ
Law laaa an tadaara kahoo ni'matum mir rabbihee lanubiza bil'araaa'i wa huwa mazmoom
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
- 68:50
فَٱجْتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Fajtabaahu rabbuhoo faja'alahoo minas saaliheen
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
- 68:51
وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَٰرِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا۟ ٱلذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجْنُونٌۭ
Wa iny-yakaadul lazeena kafaroo la-yuzliqoonaka biabsaarihim lammaa saml'uz-Zikra wa yaqooloona innahoo lamajnoon
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
- 68:52
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌۭ لِّلْعَٰلَمِينَ
Wa maa huwa illaa zikrul lil'aalameen
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
About Surah Al-Qalam
Al-Qalam, the Pen, opens with an oath by the pen and what is written, and defends the Prophet (peace be upon him) against the insult that he was mad, affirming instead that he was of the highest character. It tells the parable of the owners of a garden who were humbled, and calls for patience and steadfastness.
Themes: The pen and writing, The Prophet's character, The owners of the garden, Patience
Arabic: Uthmani script (Hafs). Translation: Swahili. Recitation: Mishary Rashid Alafasy. See Sources for full attribution.